Tuesday, February 28, 2017

LG Wazindua Simu Inayotumia Sikrini (Screen) Mbili


LG imezindua simu mpya ambayo skrini yake ni kubwa na ambayo inaweza kutumiwa njia tofauti kwa wakati mmoja.

Simu hiyo LG G6 ina mfumo wa 18:9 badala ya mfumo wa 16:9 ambao unatumiwa na simu nyingi.

Hii ina maana kuwa skrini hiyo inaonekana kubwa kuliko kawaida.





LG imekiri kuwa simu iliyozinduwa awali ya G5 ilishindwa kufikia malengo yake ya mauzo.

LG inasema kwa simu hiyo haiwezi kuathiriwa na maji wala vumbi
Simu hiyo ilizinduliwa mjini Barcelona kabla ya kuanza kwa mkutano wa simu za mkononi duniani.

Skrini ya LG G6 ina upana wa sentimita 14.5 ikilinganishwa na skrini ya sentimita 13.5 ya LG5.

Simu hiyo mya pia inawewa kuzamishwa ndani ya maji hadi muda wa nusu saa bila ya kukumbwa na tatizo lolote.
Skrini hiyo imetengenezwa kuonyesa sehemu mbili wakati mmoja
G6 ni ndogo kuliko G5 lakini skrini yake ni kubwa

Pata Makala Zetu Kwenye Simu Yako Kupitia Android Application ya Romanus Technology, Bonyeza Hapa Kuinstall

Maoni yako Hapa chini

Usipitwe Na Hii

Jinsi Ya Kupata "Likes" Nyingi Facebook

Watumiaji wengi wa facebook wamekuwa wakitamani kupata LIKES   nyingi kwenye status na picha zao wanazo post facebook lakini wameshindwa...

Back to Top
Loading...